14 June 2021
MAISHA YA GRACE MARKO SHAIDI ( Mrs. MUNGWE)
Nilizaliwa tarehe 20/04/1958 katika kijiji cha Vudee,wilaya ya Same,nikiwa mtoto wa sita wa Bw/Bi Marko Chalambo Shaidi .Namshukuru sana Mungu kwa kunipa familia kubwa na iliyo jaa upendo na furaha,Ninakumbuka utoto wangu kwa tabasamu .
Nilipata elimu ya msingi kwenye shule tofauti nne ikiwemo Vudee Indini.kuhamahama huko kulitoka na na uhamisho wa kikazi wa baba yangu ambaye alikuwa mwalimu.Licha ya ugumu ulioambatana na kuhama huko ,nilipata muda mzuri sana wa kuishi na baba yangu na kuwa na mahusiano ya karibu naye
Mwaka 1973-1978 nilipata elimu ya sekondari katika shule ya wasichana Msalato ( Dododma) na Korogwe (Tanga) .Bado nakumbuka siku niliyosafiri kwa mara ya kwanza nikitoka Kondoa kwenda Dodoma mjini peke yangu. Basi la abiria tulilosafiria liliharibika njiani na by the time tunafika maeneo ya Msalato ilikuwa ni usiku wa manane. Licha ya kusisitiza nishushwe kwenye kituo cha Msalato baadhi ya abiria walipinga na kumkataza dereava kunishusha na wanafunzi wengine wawili ambao nao pia walikuwa wanakwenda kuanza kidato cha kwanza.Ndipo mama mmoja na mumewe walipojitolea kuwa watatupa malazi nyuimbani kwao na asubuhi yake watatupeleka mahali ambapo tutapata gari la shule. Miaka hiyo watoto hawakuwa wa famiia yao tu bali waliangalia na jamii . There were good people . Namshukuru sana Mungu kwa ajili ya familia hiyo. Nakumbuka pia safari nyingi za treni kati ya Dodoma na Moshi kupItia Ruvu zilikuwa safi ndefu na tulijazana saana kwenye vyumba vya treni kwa sababu shule zilifungwa kwa wakati mmoja wa treni ilikuwa ndiyo njia iliyotumiwa na Serikali kusafirisha wanafunzi.
Nilijiunga na Jeshi la Kujenga taifa (JKT)kituo cha Oljoro, Arusha mwaka 1979. Itakumbukwa kuwa huo mwaka ndio Tanzania iliingia vitani na Uganda chini ya Idd Amini. Vijana wengi wa kiume tulikuwa nao jeshini walipelekwa kutumika vitani. Haukuwa wakati mrahisi.
Nilihitimu shahada ya usanifu majengo (Architecture) katika chuo cha Ardhi ,Dsm mwaka 1983 na kupangiwa kazi kituo cha Dodoma,Mamlaka ya ustawishaji makao makuu (CDA) interestingly,nilisoma Dodoma na kurudi kufanya kazi Dodoma na baadae kuishi jirani kabisa na Msato .
Niliolewa na kupata mtoto wangu wa kwanza mwaka 1985.
Nikiwa kazini nilipata nafasi ya kusoma Masters nchini Ubeligiji mwaka 1990 na nikatunukiwa shahada ya Architecture ââ¬âHuman Settlements.
Nikiwa Ubeligiji na familia yangu nilibarikiwa kupata mtoto wangu wa pili. Niliporudi nchini niliendelia kufanya kazi CDA mpaka zoezi la kupunguza wafanyakazi lilipofanyika na mimi nikawa mmoja wa wale waliopunguzwa. Bila kujua hii ikawa ni baraka kubwa kwangu kwani Mungu alifungua milango mingine.Mwaka 1997 nilipata nafasi ya kazi ya muda mfupi katika shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi (UN Refugee Agency-UNHCR) .Mkataba wa mwezi mmoja nilioanza nao ukaendelea kuongezwa kidogo kidogo na mwaka 2000 nikapewa mkataba wa kudumu ââ¬Åindefinite contractââ¬Â ingawaje kituo changu cha kazi kilikuwa Kigoma na baadae Kibondo. Kazi yangu ilinipa nafasi kutembelea na kutumika katika makambi yote ya wakimbizi yaliyokuwa Kigoma na Kagera jumla ya makambi kumi na moja . Kazi kubwa ilikuwa ni kutengeneza michoro ya makambi na majengo pamoja na kusimamia utekelezaji wake .Nilifurahia kazi yangu na kuifanya kwa bidii na uadilifu.Wakati wote nilimtegemea Mungu na mkono wake haukupunguka kwangu. Kwa mara ya kwanza mwaka 2003 mwanzoni niliomba kazi nje na nilichaguliwa kwenda Sierraleone. Mwaka hadi mwaka Mungu aliniinua kutoka ngazi moja hadi nyingine. Nilifanya kazi katia nchi mbalimbali mpaka mwaka 2020 nilipostaafu. Ni mwaka mmoja sasa umetiamia.Muda niliofanya kazi katika nchi ya Somalia umeacha kumbukumbu isiyosahaulika kwa urahisi moyoni mwangu. Kipindi hicho nchi ilikuwa kwenye vita na athari (risks) za utekaji nyara zilikuwa kubwa sana kazi yangu ilinihitaji kusafiri ndani ya nchi hiyo kutoka utawala mmoja kwenda mwingine na kwa hakika ni mkono wa Bwana ulionilinda wakati wote.
Nilipokaribia kustaafu nilidhamiria moyoni mwangu kuwa Mungu akinisaidia nimalize muda wangu wa ajira na kuweza kurudi nyumbani salama ,nitamtolea shukurani katika usharika wa Vudee .Ikumbukwe kuwa wakati huo ugonjwa wa COVID-19 ulishaanza na nilikaa kwenye qurantaine kwa miezi mitatu nikiwa India ââ¬âkituo changu cha kazi cha mwisho .Isingekuwa kwa serikali ya Tanzania kutuma ndege yake India kuwawazesha raia wake waliokwama nchini india kurudi nyumbani,ingechukuwa muda mrefu kupata jinsi ya kurudi Tanzania.Naishukuru sana serikali yangu .
Kwa neema ya Mungu mnamo tarehe 04/04/2021 nilipata kibali na kuweza kutimiza ahadi ya kumtolea Mungu wangu shukurani .Namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kwenda Vudee kwa ajili hiyo .Vilevile namshukuru sana Mungu kwa ajili ya ndugu zangu wote walionizingira na kushirikiana pamoja nami baraka hii .Hakika tuliuona mkono wa Bwana na tulipata muda mzuri wenye wingi wa furaha pamoja. Neno la shukrani lilitoka katika kitabu cha Zaburi 28:6-7 na Wimbo tuliouchagua ni kutoka kitabu cha Mwimbieni Bwana namba 405,(Mbele ninaendelea).
Kipindi hiki baada ya kustaafu kinaendelea kuwa cha baraka sana na kinanipa muda wa kuwa karibu na familia yangu hasa watoto na wajukuu zangu, lakini pia kushiriki katika shughuli za ukoo wangu.zaidi ya yote napata muda mzuri wa kumtumikia Mungu kwa vitendo.
Ninamaliza kwa kuwashukuru sana mabinti zangu kwa uvumilivu wao katika kipindi chote ambacho nimekuwa nafanya kazi mbalimbali
Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na Hata Milele ,Zaburi 113 :2
Bofya hapa kupata picha na video za tukio hili- https://drive.google.com/drive/folders/1Pk3GUEKhxbGY80LOuAau7AF7RhnHijaH?usp=drive_link
Ndungu zangu wapendwa katika Bwana wetu Yesu Kristo.Nimefurahishwa sana na Grace kwa kuchagua fungu jema.Amechagua kumshukuru Mungu kwa kuwa ni mwema na fadhali zake ni za milele.Ameuona ukuu na uweza wa Mungu katika maisha yake.Twendeni Vudee tuungane naye kumtolea Mungu sadaka za shukrani kwa kuwa amejaa utukufu, heshima na adhama ni mwingi wa rehema na sio mwepesi wa hasira.Siku hiyo tutatoa pia ile sadaka tuliyotoa siku ya kikao cha Marko's kilichofanyika nyumbani kwake.Tutaimbaje wimbo mpya ugenini? Zaburi 137:4 "Tuuimbeje wimbo wa BWANA katika nchi ya ugeni ? Karibuni nyumbani Vudee tusimulie mate ndo makuu ya Mungu aliyotutendea katika maisha yetu.Mungu alibariki tendo hili na azitakabali sadaka zetu.
Ndugu zangu,
Ninawasalimuni wote katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Ninaandika message hii kwa moyo wa unyenyekevu sana nikimshukuru Mungu kwa baraka zake kwetu. Tendo la kumtolea Bwana shukrani tarehe 4 April 2021 lilienda vizuri sana chini ya mkono wake wenye nguvu. Tulikuwa na vipindi vizuri vya kujifunza neno la Mungu, kuomba, kuimba na kusifu. As a family, tulipata pia muda mzuri wa kuwa pamoja na kufurahi.
Basi ninawaomba wote mpokee shukrani zangu kwenu kwa upendo na ushiriki wenu katika kutimiza kusudi la moyo wangu na nadhiri niliyokuwa nimeiweka mbele za Mungu. Nilifurahi sana kusimama madhabahuni pa Mungu nikiwa nimezungukwa na ndugu zangu na kujua kuwa hata wale walioshindwa kuja Vudee walisimama nami katika maombi na shukrani. Asanteni sana.
Wifi Marge na kaka Vince walinifanyia surprise ya cake. It was indeed a surprise. Asanteni.
Eddy na Rachel, ninawashukuru sana kwa kujitoa kubakia Vudee wakati wengine tulipoondoka ili kuiweka nyumba yetu...Holiday Home kwenye hali nzuri ya usafi. Ninawashukuruni sana.
Basi, Mungu mwenyewe atubariki sisi na vizazi vyetu. Tuzidi kupendana, kusaidiana na kuombeana katika mambo yote. UPENDO ni amri ya Mungu kwetu.
I can't thank you enough.
Nahavacheni mno.