• elisheshe@yahoo.com
  • +255765837485
service photo

NENO LA SHUKRANI KWA WAZAZI WETU SIKU YA SHAIDI DAY ILIOFANYIKA TAREHE 06/04/2019 NYUMBANI KWA WILFRED A. SHAIDI.

Tunapenda kutoa shukrani  za dhati  kutoka mioyono mwetu  kwa wazazi wetu  wakina baba, mama,shangazi na wajomba zetu  kwa malezi mazuri  mliotupatia kiroho, kiellimu, kiuchumi, kijamii na msisitizo  wenu mkubwa  katika kuimarisha undugu huu. Tunaaini  kuwa kama msingesimama  imara baadhi yetu tusingekuwa hapa  tulipo sasa.

Tunashukuru  kwa juhudi za dhati kabisa ambazo zilifanywa  na babu zetu nanyi mkaweza  kuziendeleza  kwa kuhakikisha kuwa mmeuweka  ukoo pamoja. kwa kutambua kazi  hii nzuri  mliyo ifanya  na mnaendelea  kuisimamia  tunaomba Mwenyezi Mungu  awabariki sana.

Tunafahamu pia changamoto  zilizoko sasa za kutuweka  pamoja  ni kubwa kushinda ilivyokuwa  mwanzo kwa sababu zifuatazo:

ØUkoo umepanuka sana kwa sababu wako ndugu ambao wameoa  na kuolewa sehemu mbalimbali za nchi

ØWanaokoo pia  wanaishi maeneo mbali ya nchi kwa sababu mbalimbali za kimaisha.

Kutokana  na sababu hizo hapo juu, wakati huu  ndio wakati tunahitaji  kushikamana  na kushirikiana  zaidi kuliko ilivyokuwa  hapo awali. Mungu azidi  kutuimarisha   kiroho ili kila mmoja  wetu aweze  kutambua nafasi yake  katika familia  hii. Lengo  la kila  mmoja wetu liwe kuhakikisha  kuwa umoja huu unaimarika.

Hivyo basi wapendwa baba, mama, shangazi, na wajomba zetu ili ukoo wetu uendelee kuimarika  tunaomba  kwa heshima  mpokee mapendekezo yetu ambayo tumetoa ili na sisi kizazi chetu kiweze kuwa enzi wazee wetu kwa kuweka  ukoo pamoja hadi na sisi tukapokabidhi kwa watoto wetu ikiwa shaidi moja ambayo haijameguka, na mapendekezo yetu yatawasilishwa  kwenu kama ifuatavyo:

MAPENDEKEZO:                                                                                                                  WASEMAJI:

1:KUWE NA UWIANO SAWA KATIKA USHIRIKI WA MATUKIO                           -MRS ANNA NGOO

2: UPENDO USIO NA UBAGUZI                                                                                      -MRS JENIFER ITOSI

3:KUWA NA UTARATIBU  MZURI WA KUENDESHA VIKAO                                 -MR KILONZO MCHOME

4:KUWE  NA UTARATIBU MZURI WA KUPEANA TAARIFA (WAZEE VS VITUKUU)     -MRS NELLY LYARUU                             


Picha za tukio hili zinapatikana kwa kubofya hapa- Shaidi Day 2019