KUMSHUKURU MUNGU KWA MOYO WAKO WOTE
Kumshukuru Mungu kwa moyo wako wote maana yake ni nini? Kuna njia mbili za kushukuru unaweza kushukuru kwa maneno na vitendo vya nje ambavyo humaanishi ni kama kiili macho au kama kawaida ya mtu akitendewa jambo jema. Shukrani za aina ya pili ni zile zinazotoka ndani ya myo wako .Maneno na vitendo vyako vya shukrani vinasukumwa na moyo wako au tusema ni shukrani inayoanzia moyoni ndio viashiria vya nje vitokee kama vile kicheko, furaha na mashangilio. Hizi ndizo shukrani zinazompendeza Mungu. Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu (2 Wakorintho 9:7). Tutoe shukran kwa Mungu kwa moyo wa kupenda wala sio wa kulazimishwa au kushurutishwa au kwa masharti yoyote yale. 2 Wakorintho 9:7 “Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake si kwa huzuni wala si kwa lazima,Maana Mungu humpenda yeye atoaye shukrani kwa moyo wa ukunjufu”. Mtu anayetoa kwa moyo wa ukunjufu anampenda Mungu kwa moyo wake wote .Neno la Mungu katika Luka 10:27(a) linasema “akajibu akawambia,(Yesu Kristo),Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote.”Moyo wa shukrani ni moyo unaomrudishia Mungu utukufu na heshima zote.Ukiwa na moyo wa shukrani utajikuta unamwinua Mungu kwa kuelezea kwa watu na makutano juu ya uweza wake na nguvu zake na matendo yake makuu na ya ajabu. Zab:35-18. “Nitashukuru katika kusanyiko kubwa, nitakusifu kati ya watu wengi.” Na sisi kama Daudi tumshukuru Mungu kati ya watu na kati ya mataifa. Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu maana yeye atatuwesha .Jina la BWANA Lihimidiwe tangu leo na hata milele.